Monday 1 February 2021

Kolabo za Nandy zinasema jambo kuhusu Wasafi!

 Kwenye moja ya mahojiano ya gazeti la Mwananchi na msanii wa muziki wa Bongofleva, Faustina Mfinanga ‘Nandy’ aliulizwa, je, kuna bifu kati yako na lebo ya Wasafi? Nandy akajibu “hapana.”

Akaulizwa, je Wasafi ni washindani wako namba ngapi kwenye orodha ya wapinzani wako, akajibu yeye hafanyi muziki kushindana na mtu yeyote, sio Wasafi wala sio lebo yoyote chini, bali anafanya muziki kwa nafasi yake.

Hayo yalikuwa majibu mazuri kutoka kwa Nandy na huenda yamejaa ukweli tupu, lakini ubaya ni kwamba matukio yanayoendelea kati ya Nandy na Wasafi yanakinzana na majibu.

Matukio yanaonyesha pande mbili hizo zina ushindani na hata kama haupo hawana budi kuukubali kwa sababu unatoka mtaani kwa mashabiki. Na kwa sababu hiyo, leo tunaangalia jinsi kolabo zinazomfanya Nandy na Wasafi kuwa kama Simba na Yanga, jinsi zinavyothibitisha kuwa kweli wawili wana lao.

Kolabo na Harmonize

Miezi sita tangu msanii Harmonize atangaze kujivua ngozi ya WCB alinaswa na Nandy na wakafanya kolabo na ikawa ni wimbo gumzo mtaani. Wimbo unaitwa Acha Lizame na mpaka sasa umekusanya watazamaji zaidi ya milioni 7 kwenye Youtube.

Wimbo huo ulikuwa ni moja ya matukio yalichatiza kuwa huenda ni kweli Nandy na Wasafi wanapigana vikumbo kwa sababu kwa kipindi chote cha maisha ya muziki wa Nandy hakuwahi kusikia kolabo yake na msanii kutoka Wasafi licha ya kwamba wengi anaendena nao kimuziki.

Labda hawapo kwenye mipango yake, lakini mbona mara tu baada ya Harmonize kujitoa WCB alimdaka na kufanya naye kazi? Hiyo ilitafsirika kuwa kumbe Nandy alikuwa anatamani kufanya kazi na mastaa wa Wasafi au mastaa wa Wasafi wanamtamani Nandy lakini matamanio nayo yanashindwa kuwa kweli kwa sababu pande mbili hizo zina mvutano.

Kolabo na Joeboy

Tangu Wasafi wamtambulishe malkia wao Zuhura Kopa ‘Zuchu’, Nandy amekuwa akishindanishwa sana na mkali huyo wa wimbo wa Sukari. Ni ushindani ambao haukwepeki kwa sababu wanafanya muziki wa aina moja Bongofleva, jinsia moja wanawake, umri sawa miaka 27 kwa 28 pia wote wanaimba vizuri.

Sasa miezi miwili iliyopita Zuchu alitoa wimbo wa mwisho kwa mwaka 2020 ukaitwa Nobody akimshirikisha msanii kutoka Nigeria, Joeboy. Halafu wiki nane zilizofuata Nandy naye akaachia wimbo ukaitwa Number One akiwa amemshirikisha Joeboy.

Hiyo ilitengeneza taswira ya kwamba huenda ni kweli wawili hawa wana upinzani ambao hawataki kuusema kwa maneno, bali matendo.

Huyu akifanya hili huyu anafanya lile kama Simba na Yanga. Matokeo yake ni kwamba imechochea zaidi kushindanishwa. Na sasa watu sio tu wamepata fursa ya kushindanisha Nandy na Zuchu, bali wanashindasha wimbo wa Nandy na Joeboy na Zuchu na Joeboy.

Kolabo na Koffi

Kubwa kuliko ni kwamba hivi majuzi Nandy alikuwa pale Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kumpokea Koffi Olomide kwa ajili ya kuja kufanya naye video ya wimbo wao ambao tayari wameutengeneza na kuupa jina la Leo.

Mbaya zaidi ni kwamba tukio hilo limetokea wiki nne tangu msanii wa Wasafi, Diamond Platnumz naye ampokee Koffi nchini kwa ajili ya kurekodi naye wimbo unaoitwa Waah ambayo tayari umetoka na kuvunja rekodi kibao.

Hii inaendelea kutengeneza sababu za mashabiki kuamini kwamba huenda ni kweli pande hizi mbili yaani Nandy na timu nzima ya WCB wana ushindani.

Kolabo na Alikiba

Iko wazi kwamba mpinzani namba moja wa Dimaond na WCB nzima ni Alikiba, labda sio jambo rasmi lakini angalau ndivyo inavyofahamika na watu wengi. Na mara kadhaa imeonekana kuwa wasanii wanaoweza kufanya kolabo na Alikiba ni wale ambao wanaonekana hawana ukaribu na WCB. Mfano wa wasanii hao ni Aslay, Darassa na sasa Nandy anaingia kwenye orodha hiyo kwa sababu miezi miwili iliyopita aliachia wimbo wa Nibakishie alioshirkiana na Alikiba.

Kuhusu ushindani

Ukitazama biashara zote zilizofanikiwa duniani zilifanikishwa na mambo mawili makuu. Kwanza bidhaa nzuri, pili ushindani. Bidhaa ya Nandy na Wasafi ni muziki, na kwa hakika pande mbili hizi zinafanya muziki mzuri. Kwa hiyo kinachokosekana hapa ni ushindani ambao mpaka sasa umebaki kama tetesi kwa sababu hakuna ambaye amekiri kuna ushindani.

Saturday 9 January 2021

Mastaa hawa wana dalili za kuaga ukapera 2021

 Mwaka jana zaidi ya mastaa nane walifunga ndoa. Mwaka huu ni kina nani wataingia kwenye safina hiyo ngumu kuchonga? hapa nakupa uchambuzi wa mastaa wenye dalili ya kufunga ndoa mwaka 2021 ikiwa ni pamoja na asilima za uwezekano wa kuwepo kwa ndoa hizo kwa kila msanii husika.

SHILOLE 95%

Shishi Biden alimaliza mwaka 2020 akiwa na pete ya uchumba kidoleni aliyovalishwa na bebi wake mpya, mpiga picha anayefahamika kwa jina la Rommy 3D.

Kwanini tunadhani Shilole ana 95% ya kufunga ndoa mwaka huu? Ni kwa sababu kwanza ana pete ya uchumba tayari, pili Shilole mwenyewe anakiri kuwa kwa hatua aliyofikia sasa hawezi kuwa na mpenzi tu bila ndoa, ana watoto wakubwa, ana majukumu makubwa, hawezi kuvumilia mapenzi ya ujana ujana kwahiyo kwake ndoa ni kitu muhimu kama kitambulisho ya Nida.

Tatu, Shishi Baby na mpenzi wake wa sasa wana historia kubwa sana ya mapenzi, ambayo walisimulia wenyewe kupitia Instagram zao kwamba walikuwa wapenzi zamani na mipango yao ilikuwa ni kuoana lakini waliachana kutokana na sababu za kimaisha, sio kwamba waligombana au walitengana kwa shari. Na kwa sasa wako pamoja na kwa kuwa hizo sababu za kimaisha hazipo tena, kwahiyo ni kitu gani kinaweza kuwazuia wasifunge ndoa mwaka huu?

Nne ni hata ukipita Instagram zao, utagundua kuwa mahaba yao ni ya moto kweli kweli. Mmoja asipokula mwingine chakula hakishuki kooni. Na hivi tunavyozungumza Shilole amempeleka mumewe mtarajiwa kwao Igunga kwa ajili ya kumtambulisha kwa wakwe na mashemeji.

Pia Shilole anaweza kuamua kuolewa ili amuumize moyo mumewe wa zamani Uchebe ambaye mpaka sasa bado wanapigana vijembe huko mitandaoni. Sio sababu nzito lakini ni nani anayeweza kuelewa akili za wasanii zinavyofanya kazi? Ziko tofauti sana.

VANESSA MDEE 80%

Masaa machache kabla ya kuingia mwaka mpya 2021 Vanessa Mdee alipewa zaidi ya kuvalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake, muigizaji wa Marekani mwenye asili ya Nigeria, Olurotimi Akinosho ‘Rotimi’.

Tunadhani Vee Money ana asilima 80 ya kufunga ndoa mwaka huu na Rotimi wake kwa sababu tayari ana pete uchumba. Pili yeye na Baby wake mapenzi yao yamenoga kama ya Adamu na hawa uko Instagram. Ukiingia tu unakutana na picha, wamepostiana, hujakaa vizuri hao wapo wanafanya video live, ni shida.

Tatu Rotimi mwenyewe anadai Vanessa ni mtu sahihi zaidi kuwa mke wake kwa sababu alikaa naye ndani kipindi nchi ya Marekani ipo kwenye ‘lockdown’ ya corona, kwahiyo anaamani kama aliweza kufurahia naye maisha wakiwa wawili tu bila kuboreka, maana huyo ni mtu sahihi kwa ajili ya maisha yake yote.

Na nne, wakati anafanya Instalive hivi majuzi Januari 4, shabiki mmoja alimuuliza kuhusu mipango yao ya kufunga ndoa, Vanessa alijbu itafanyika hivi karibuni.

Kama hiyo haitoshi, aliulizwa kuhusu mtoto, akasema wanatazamia kupata mtoto kabla ya mwaka huu kuisha. Hii ni sawa na kusema utajuaje kama wamepanga kupata mtoto wakiwa tayari kwenye ndoa? Kwahiyo kama mtoto atapatikana mwaka huu kuna uwezekano mkubwa ndoa ikawa mwaka huu pia.

BILLNAS & NANDY 70%

Kila mtu anajua kuwa tayari Billnas alishamvisha pete Nandy. Pete ambayo baadae familia ya Nandy ilikataa kuitambua kwa sababu haikufuata taratibu; waliwalishana jukwaani.

Hata hivyo Billnas akaona isiwe poa, akatuma wazee waende kwa kina Nandy kujitambulisha na wakafanya hivyo. Na kwa mujibu wa Nandy mwenyewe aliandika kwenye Instagram yake kuwa barua ya Billnas iimepokelewa na kupata majibu mazuri.

Kinachofuata baada ya hapo ni ndoa tu na ndiyo maana tunasema kuna 70% za ndoa hiyo ikafanyika mwaka huu 2021.

ELIZABETH MICHAEL 55%

Aisee! Elizabeth Michael ‘Lulu’ anatembea na pete ya uchumba aliyovishwa na Majizo kwa zaidi ya miaka miwili sasa mpaka mashabiki zake wamechoka kiasi kwamba akipost chochote kwenye Instagram yake watu huandika kumuuliza kuhusu anaolewa lini.

Unaambiwa mpaka aliyekuwa mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda alikuwa muangalizi wa uhusiano huu kuanzia mwaka 2018 lakini mwaka ukapita bila ndoa, 2019 ikapita na 2020 pia ikapita bila mchumba wa Lulu ambaye ni mmiliki wa EFM na ETV kufunga ndoa na mdogo wetu.

Pia inadaiwa Oktoba mwaka jana ndoa ya wiwili hao ilitangazwa Kanisa Katoliki la Mtakatifu Andrea Bahari Beach jijini Dar es Salaam. Hilo lilikuwa tangazo la kwanza na kwamba, baada ya wiki mbili mbele ilitakiwa wawili hao waunganishe miili kuwa kitu kimoja, lakini mwaka uliisha bila hilo kuwekezekana.

Sasa kwa sababu haifahamiki wazi wazi ni nini haswa kilikwamisha washindwe kufunga ndoa mwaka jana, bila shaka kuna nafasi kubwa ya wao kufikia utatuzi na ndoa ikawezekana mwaka huu.

DIAMOND 51%

Mwaka jana ilibaki kidogo tu Diamond amuoe mama wa mtoto wake wa mwisho, muimbaji kutoka Kenya, Tanasha Dona. Kulikuwa na viashiri vyote lakini hata yeye mwenyewe aliwahi kuzungumzia utayari wake katika hilo. Lakini sijui Tanasha alimchokoza nini kaka yetu, wakatemana na mipango ya ndoa ikafia huko.

Na ndani ya mwaka 2020 karibu kila mtu wa karibu wa Diamond alikuwa akimsukuma kuoa. Meneja wake walikuwa wakimpiga vijembe aoe, dada zake Esma na Queen Darleen, hata mama yake na baba zake wote wawili, ,mzazi na wa kufiki wanaonesha kutumani kuona mtoto wao akioa kwa mwaka jana. Hata hivyo kwa sababu hilo lilishindakana 2020, kabda litawezekana mwaka huu; hata hivyo jamaa haeleweki kwenye mambo ya mahusiano ndiyo maana ndoa yake inatazamiwa kwa asilimia 51 tu.



Wednesday 20 March 2019

Mapya yaibuka ndoa ya Bieber na mrembo Hailey

Ndoa ya staa wa muziki wa RnB na Pop, Justin Bieber na mpenzi wake Hailey Baldwin iliyokuwa ifungwe ndani ya mwezi ujao imesogezwa mbele hadi pale watakapo tangaza tena.

Kwa mujibu wa TMZ, umeripoti kuwa wapenzi hao wamelazimika kuipeleka mbele ndoa yao kwasababu za kiafya zinazomkabili nyota huyo. TMZ ilielezwa na chanzo cha karibu cha nyota huyo.

Iliripotiwa kuwa, Juma lililopita msanii huyo alipost picha yenye ujumbe wa kuwataka mashabiki wake wamuweke kwenye maombi kwani anapitia changamoto ya kiafya japo hakutaka kuweka wazi ni ugonjwa gani.

Hadi sasa hii imekuwa mara ya nne wapendanao hao wamekuwa wakihairisha ndoa yao kwasababu mbalimbali zisizowekwa wazi.

“Watakuwa na harusi hatimaye, lakini hii sio lengo lao sasa,” kwa mujibu wa chanzo kilichoiambia TMZ. “Wao watasubiri mpaka Justin atakapojisikia vizuri na anafurahi juu ya kupanga ndoa yao tena.

Mwezi uliopita, ni wazi kwamba Justin alikuwa anapokea matibabu kwa ajili ya unyogovu kwa sababu amekuwa amejeruhiwa na umaarufu hivi karibuni. ukweli ni kwamba mashabiki hutengeneza kila hoja, nk. Yeye bado anapokea matibabu, ndiyo sababu harusi sio kipaumbele cha juu kwa wanandoa. Justin bado anapokea matibabu kwenye pwani zote mbili lakini muda sio mrefu atakuwa sawa,” chanzo hicho kinasema.

“Yeye sana, anazingatia kupata nafuu. Anataka kuwa mahali pazuri kwa ajili yake na Hailey. Yeye bado ana imani kwamba atafunga ndoa.“

Thursday 28 September 2017

Fahamu jinsi ya Ku-bet

GG (maana yake tim zote zifungane).. GGGG ( tim zote zifungane kila kipindi)

2+ (katika mechi yote yapatikane magoli kuanzia mawili)...

I 2+ (kipindi cha kwanza yapatikane magoli kuanzia mawli)...

II2+ (kipindi cha pili yapatikane magoli kuanzia mawili)....

H2+ (tim ya nyumbani ipate magoli kuanzia mawili)...

A2+ (timu ya ugenini ipate magoli kuanzia mawili)...